Theme images by MichaelJay. Powered by Blogger.

Visitors

Search This Blog



Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Youtube



Flickr Images

Like us on Facebook

Instagram

Facebook

Tuesday, April 17, 2018

Wanawake waaswa kujifunza matumiz sahihi ya mitandao na kujifunza zaid k...



NA EUNICE ROBERT

Wanawake kote nchini wameaswa kujifunza matumizi sahihi ya mitandao ili kukua kiteknolojia kwani kuna umuhimu wa kutumia teknolojia kwenye karne hii ya ishirini na moja.

Akizungumza na Lens Media Tv mkurugenzi wa Zaina Foundation Bi.Zainab amesema kuwa wasichana na wanawake wamekuwa nyuma sana kwenye matumizi ya teknolojia na pia hawapewi nafasi ya kuweza kujifunza ili kujua mambo mbalimbali yanayohusu  teknolojia.

Ameongeza kwa kusema kuwa endapo watapata uelewa wa jinsi ya kutumia teknolojia wanaweza kutumia kwa kusoma na kwenye maswala ya afya.

Ameendelea kusema kuwa wanatarajia kila kitu kitumike kwa kuzingatia teknolojia inavyokuwa hivyo wamefanya semina na wanawake ili kuwapa elimu hiyo ya kutumia teknolojia.

Kwa upande wake Bw.Frank Nduguru ambaye ni mmoja wa washiriki amesema kuwa wamejifunza mambo mengi kuhusu Cyber Crimes na kutumia teknolojia kwa matumizi sahihi na sio kutuma picha zisizo na maadili kwa jamii ya kitanzania.

Nae Bi,Magdalena Mhina amesema kuwa wanatarajia kuwa wasichana watajilinda kuhusiana na maswala ya uzazi ili kuweza kufikia malengo yao kwa kutumia teknolojia kwa usahihi


No comments:
Write comments

Interested for our works and services?
Get more of our update !