NA EUNICE ROBERT,
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mh,Mashaka Mrisho Gambo,amewataka wananchi kuwa na vitambulisho vya Taifa mapema hii leo katika eneo la soko kuu mkoani Arusha.
Wakati akizindua rasmi zoezi la vitambulisho vya Taifa Mh,Gambo amesema kuwa lazima kila mtanzania awe na kitambulisho hicho kwani ndicho kitakachompelekea kufahamika kuwa yeye ni raia wa Tanzania.
Mh,Mashaka amehitimisha kwa kuwataka wananchi wote wa mkoa wa Arusha kuhakikisha wanapata vitambulisho hivyo kwani vitawasaidia kupunguza uhalifu katika jiji la Arusha
No comments:
Write comments