NA EUNICE ROBERT
katibu wa TUGHE na mratibu wa TUCTA mkoa wa Arusha Bw.Samwel Magero amesema kuwa mwaka huu wanategemea kuwa na sherehe za mei mosi na wamejipanga vizuri na uongozi wa serikali na pia wameshaanza maandalizi mbalimbali kwa ajili ya sherehe hizo zinazotarajiwa kufanyika kitaifa mkoani Arusha.
Bw.Magero amesema kuwa wamejiandaa vyema kukamilisha sherehe hiyo na mgeni rasmi anayetarajiwa kuwepo ni raisi wa nchi Mh.John Pombe Magufuli,hivyo ametangaza rasmi kwa wananchi wa Arusha kuwa tarehe moja mwezi wa tano sherehe za mei mosi zitafanyika kitaifa mkoa wa Arusha hivyo amewataka wananchi wote waweze kushiriki katika sherehe hizo.
ameendelea kusema kuwa kabla ya mei mosi kutakuwa na maonyesho ya OSHA kuanzia tarehe ishirini na tano ambapo wataonyesha mambo mbalimbali yanayohusu mambo ya kazi na mfuko wa hifadhi ya jamii.
Bw.Magero ametoa rai kwa wananchi na wafanyakazi waweze kufika kwenye maonyesho hayo ili waweze kujifunza mambo mbalimbali watakayokuwa wameandaa
No comments:
Write comments