mratibu wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania TUCTA mkoa wa Arusha Bw.Samwel Marero.
Wafanyakazi na waajiriwa wa serikali na sekta binafsi wametakiwa kutumia sikukuu ya wafanyakazi ulimwenguni kwa kutafakari na kuboresha majukumu yao badala ya kuibua changamoto na mapungufu yanayojitokeza sehemu za kazi.
Rai hiyo imetolewa leo na mratibu wa shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania TUCTA mkoa wa Arusha Bw Samwel Marero Magero.
Bw.Marero amesisitiza wafanyakazi na waajiriwa wanapaswa kuwa kitu kimoja ili kuleta ufanisi kazini na kuwataka kujitokeza kwa wingi ili kufanikisha sherehe hizo pamoja na kupata muafaka wa changamoto zao kwa ujumla.
kwa upande wake katibu wa chama cha wafanyakazi viwandani TWIKLE kanda ya kaskazini Bw.Hussein Ngowo wao kama waandaaji rasmi wa maadhimisho hayo wanahakikisha wanafanya uhamasishaji wa hali ya juu kufanikisha sherehe hizo.
Ameongeza kuwa tayari wameunda kamati ya maandalizi kwa kushirikiana na serikali kupitia ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha
Maadhimisho ya sikukuu ya wafanyakazi mei mosi huazimishwa kila mwaka tarehe moja mwezi wa tano ambapo wafanyakazi ulimwenguni kote hutumia siku hiyo kutafakari na kutatua changamoto mbalimbali katika sehemu zao za kazi.
No comments:
Write comments