NA EUNICE ROBERT.
ARUSHA
Mwanasheria wa chama cha mapinduzi (CCM) Bw.Ngemela amesimamia zoezi la kufanya usafi katika kiwanja kilichokuwa kimetaifishwa ambacho ni mali ya chama hicho.
Akizungumza na Lens Media Television mwenyekiti wa kata ya Themi Bw.Thomas Munisi amesema kuwa hawako tayari kuendelea kuona baadhi ya viongozi kutumia mali za chama kwa njia isiyo sahihi.
Hata hivyo ameongeza kwa kusema kuwa kundi la vijana wamejitokeza kufanya usafi katika kiwanja kilichothibitishwa na mwanasheria wao Bw.Ngemela kuwa ni mali halali ya chama hicho
Aidha Bw.Thomas ameendelea kusema kuwa wamejipanga vizuri na wameeka mikakati ya kuhakikisha chama chao kinasimama imara na kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi.
Amehitimisha kwa kuwataka wanachama na viongozi wa chama cha mapinduzi kuwa waaminifu kwa kuzilinda mali za chama hicho.
No comments:
Write comments