Theme images by MichaelJay. Powered by Blogger.

Visitors

Search This Blog



Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Youtube



Flickr Images

Like us on Facebook

Instagram

Facebook

Thursday, April 5, 2018

MAGUFULI KUZINDUA NYUMBA ZA POLISI ZILIZO JENGWA BAADA YA KUUNGUA MWAK...





NA EUNICE ROBERT

Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt John pombe Joseph Magufuli anatarajiwa kufungua kituo cha polisi cha kisasa cha kwanza hapa nchini siku ya jumamosi  kitakachotoa huduma kwa watalii na wanadiplomasia jijini Arusha.

Hayo yamebainishwa na kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo wakati akiongea na waandishi wa habari ambapo amesema kuwa pamoja na mambo mengine raisi atazindua nyumba za askari zilizopo kituo cha polisi cha kati.

Bw.Charles ameendelea kusema kuwa siku hiyo kutakuwa na maonyesho ya utendaji kazi wa jeshi la polisi mkoa wa Arusha yatakayofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid  hivyo ametoa wito kwa wananchi na wakazi wa Arusha kufika bila kukosa ili kushuhudia uimara wa jeshi la polisi.

Aidha ameongeza kuwa nyumba za polisi zimekamilika na mara baada ya kufunguliwa zitaanza kutumika pia ameendelea kusema kuwa kutafanyika ufunguzi wa vituo viwili vya polisi kwani hapa nchini Tanzania hakujawahi kuwa na kituo cha kidiplomasia hivyo amesema kuwa jeshi la polisi limeamua kufungua kituo kikubwa  cha kisasa kitakachofunguliwa na Mh.raisi John Pombe Magufuli.

Amehitimisha kwa kusema  kuwa kituo kingine cha kisasa cha daraja la kati ambacho kitatoa huduma kata ya Murieti kwa Morombo kitafunguliwa siku hiyo hivyo amewataka wananchi kuhudhuria siku hiyo kwa ajili ya kushuhudia ufunguzi wa nyumba hizo na utendaji kazi wa jeshi la polisi mkoa wa Arusha.






No comments:
Write comments

Interested for our works and services?
Get more of our update !