Theme images by MichaelJay. Powered by Blogger.

Visitors

Search This Blog



Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Youtube



Flickr Images

Like us on Facebook

Instagram

Facebook

Monday, April 9, 2018

MAAFA ARUSHA: mafuriko yasababisha hasara kubwa kwa baadhi ya wakaz wa m...



NA EUNICE ROBERT

Pamoja na serikali kuendelea kutengeneza mikondo ya maji ili kuepusha mafuriko lakini bado baadhi ya maeneo mkoani Arusha yameendelea kukumbwa na adha ya mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi wa mtaa wa Lolovono mkoani humo wameeleza kile kilichotokea usiku wa kuamkia leo na kusema kuwa mvua zilizonyesha zimesababisha uharibifu mkubwa na kupoteza vitu vya ndani pamoja na kukosa mahali pa kulala kwani magodoro na vitanda vimechukuliwa na mafuriko hayo.

kwa upande wake Bi Dora John  mhanga wa tukio hili amesema kuwa mafuriko hayo yamesababisha nguo za watoto wake kulowa na kupelekea kukosa nguo za kuwavalisha watoto wake pamoja na kukosa mahali pa kulala kwani nyumba zimebomoka na magodoro yamelowana.

Nae Bi Irene Izack shuhuda wa tukio hili amesema kuwa mafuriko hayo yameanza jana usiku muda wa saa nane ambapo walishtushwa na kelele zilizowafanya waweze kutafuta msaada wa haraka kwa ajili ya kuwasaidia wahanga wa mafuriko hayo

wakazi hao wamehitimisha kwa kuiomba serikali iwasaidie kurekebisha mkondo wa maji kwani maji hayo yalizidi na kukosa njia ya kutokea hivyo yalitafuta njia iliyoko wazi ambapo kuna makazi ya watu na kusababisha uharibifu wa mali zao.

No comments:
Write comments

Interested for our works and services?
Get more of our update !