NA EUNICE ROBERT
Pamoja na baadhi ya wafanyabiashara wanaotumia bandari kupitisha mizigo yao kuwa wakaidi wa kutokulipa ushuru lakini bado serikali imeendelea kufanikiwa kudhibiti hali hiyo.
Akizungumza na Lens Media Tv kaimu kamishna wa forodha na ushuru wa bidhaa Tanzania Mh.Ben Usaje amesema kuwa mradi wa kwanza waliobuni ni single custom territory ili kupunguza gharama na muda unaotumika kusafirisha mizigo kutoka badari ya mombasa na Dar-es-salaam kwenda kwenye nchi zisizona bandari.
Bw.Ben ameendelea kusema kuwa mradi huo unasaidia nchi husika ambayo mzigo unaenda kuweza kuandika ripoti ya mzigo huo kabla haujafika ikiwa na maana ya kulinda bidhaa za viwanda vilivyopo nchini.
Ameongeza kuwa wameanzisha mfumo ambao unasaidia kuwafanya wafanyabiashara kusema ukweli wa bidhaa zao bila kudanganya na kuepusha usumbufu wa kukagua na kufanya utaratibu wa kukagua mzigo kama ni wenyewe.
Amehitimisha kwa kusema kuwa bado mawakala wa forodha hawana ruhusa ya kuangalia bei na bidhaa kutoka nchi zingine ili waweze kuagiza
No comments:
Write comments